Rais Jakaya Kikwete na rais Pierre Mkurunzinza wa Burundi wamezindua mpango wa uimarishaji wa alama za mipaka ya kimataifa kati ya Tanzania na Burundi ikiwa ni utelelezaji wa agizo la umoja wa nchi za Afrika -AU-linalotaka nchi wanachama kuhakiki alama za mipaka kufikia mwaka 2017.

Akizungumza na mamia ya wananchi wa Tanzania na Burundi mpakani mwa nchi hizo wilayani ngara,rais Jakaya Kikwete amesema uimarshaji wa mipaka hauna lengo la kuwatenganisha wananchi bali kuweka utaratibu wa huduma na usalama na kuimarisha udugu na kibiashara baina ya nchi hizo.
 Kwa upande wake rais wa Burundi Mhe Pierre Nkurunzinza licha ya kutoa shukrani kwa Tanzania katika kuisaidia Burundi amewatoa shaka wananchi wa Burundi walioingiliwa na mipaka na ambapo serikali ya nchi hiyo itatafuta namna ya kuwafidia.
Awali wakizungumza katika uzinduzi huo, mawaziri wa ardhi wa nchi hizo mbili Mhe. Prof Anna Tibaijuka na bwana Jean Cloude Ndewayo wamesema kuwepo kwa milima na mabonde katia eneo la mipakani kunafanya utambuzi wa mipaka kuwa migumu kwa wananchi wa kawaida kwa kutambua tatizo hilo serikali ilianza utambuzi wa mipaka hiyo kwa vipindi tofauti.
 Uzinduzi huo uliofanyika mpakani mwa Tanzania na Burundi uliohudhuriwa na viongozi mbalimbali na nchi hizo pamoja na wananchi wanaoishi mpakani ambapo vikundi mbalimbali vya burudani na sanaa vilitumbwizi.
Share To:
Magpress

MagPress

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

0 comments so far,add yours