Baadhi ya Wafanyabiashara wa kati Mjini Morogoro wamefunga maduka yao kwa hofu ya kufungiwa  na Mamlaka ya mapato nchini TRA na kutozwa mamilioni ya fedha kama faini kutokana na kutokuwa na mashine za risiti za kielektroniki za (EFD) ,wakidai hatua hizo zimeanza kuchukuliwa  jijini Dar es salaam, huku bado mazungumzo kati ya TRA na wafanyabiashara yakiwa bado hayajakamilika.
Mwenyekiti wa wafanyabiashara wa kati mjini Morogoro, Ali Mamba amesema mgomo huo  hauhusiani na matumizi ya mashine hizo bali mfumo mzima wa ulipaji wa kodi kwa wafanyabiashara ambao pamoja na kushawishiwa kuachana na mgomo huo, wamedaai kuchukua uamuzi huo kwa  kutowaamini viongozi  wao katika mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea baina yao na TRA, kwa kushuhudia mamlaka hiyo ikianza kuwafungia wafanyabiashara jijini Dar es salaam.
Kufungwa huko amesema kunakwenda  sambamba na masharti  magumu  ikiwemo kutakiwa kulipa faini ya sh milioni tatu, kununua mashine kwa laki sita na shilingi elfu themanini ya kufuli linalotumika kufungia eneo husika linalofungiwa.
Nao wafanyabiashara wanaosambaza bidhaa katika maduka mbalimbali, walieleza kuathiriwa na mgomo huo na kwamba pamoja na kutumia mashine husika, bado mtandao wake ni wa tabu, hivyo TRA badala ya kutaka wafanyabiashara watumie mashine ni vyema ikaangalia pia na changamoto zilizopo kwenye mfumo huo kabla ya kuhimiza matumizi.
Meneja wa TRA mkoa wa Morogoro Kilomba Kanse, alikataa kuzungumzia hali hiyo kwa  madai tayari Kamishna mkuu wa mamlaka hiyo, Risherd Bade,alishazungumza na vyombo vya habari kuhusiana na mashine hizo.
Akinukuliwa na vyombo vya habari, Kamishna Mkuu wa Tra, Risherd Bade,mbali na kuzungumzia umuhimu wa  uanzishwaji wa mashine za EFD, na kuwahimiza wananchi kudai risiti sahihi kwa kiwango cha fedha wanachotoa wanunuapo bidhaa, amewaonya wanaohamasisha, kutishia au kutumia njia yoyote kuwarubuni wengine wasitumie mashine hizo ama kufunga biashara zao waache mara moja, vinginevyo sheria itachukua mkondo wake.
Share To:
Magpress

MagPress

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

0 comments so far,add yours