Jitihada za Tanzania za kusaidia kuleta ufumbuzi wa mgogoro wa kisiasa katika nchi ya Sudani kusini kwa njia mazungumzo umeanza kuonyesha mwelekeo wa mafanikio baada ya viongozi wa makundi matatu yaliyotofautianandani ya chama cha (SPLM) kusaini makubaliano ya kusitisha mapigano na kuanza mazungumzo.
Wakizungumza baada ya kusaini makubaliano hayo mbele ya marais Mh. Uhuru Kenyeta wa Kenya, Yoweri Museven wa Uganda na mwenyeji wao Mh Rais Dr, Jakaya Kikwete viongozi makundi yote yaliyotofautiana wameahidi mbele ya marais Dr, Jakaya Kikwete wa Tanzania, kuheshimu makubaliano yaliyofikiwa.
 
Kwa upande wao rais Uhuru Kenyata wa Kenya na Yoweri Museveni wa Uganda wamewataka viongozi wa makundi hayo kuona umuhimu wa kutanguliza mbele maslahi ya wananchi wao wanaoendelea kuteseka kwa sababu ya tofauti za mitazamo ambazo zinaweza kumalizika bila  kupigana, na wameipongeza Tanzania kwa kuendeleza harakati za hayati baba wa taifa Mwalim Nyerere za kumaaliza matatizo kwa njia za mazunguzo.
 
Awali mwenyekiti wa mazungumzo hayo Mh John Malechelea na katibu wa CCM iliyokuwa inaratibu zoezi hilo Mh Abdulrahaman Kinana pamoja na kueleza baadhi ya makubaliano yaliyofikiwa na pande zote likiwemo la kuheshimu uhuru na haki kila mwanachama kugombea nafasi za uongozi wamewataka viongozi hao kuwa na uvumilivu wa  kisiasa.
 
Akihitimisha kikao hicho rais wa Tanzania Mh Dr, Jakaya Kiwete amesema Tanzania itanedelea kutoa mchango wake wa hali na mali wa kupigania amani na kuhakikisha mazungumzo yanatumika kumaliza tofauti popote zinapojitokeza kwani ni jambo linalowezekana.
 
Zoezi la kuhitmisha makubaliano hayo kwa kutiliana sahihi lilitarajiwa kufanyika saa nne hadi saa tano mchana wa tarehe 21/01/2015  lakini  halikuwezekana kutokana na kuibuka kwa mvutano miongoni mwao ambao ulisababisha zoezi hilo kumalizka saa sita na robo usiku.
Share To:
Magpress

MagPress

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

0 comments so far,add yours