Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa Takukuru imewafikisha mahakamani watumishi watatu wa serikali akiwemo mkurugenzi wa fedha wa benki kuu ya Tanzania BOT Julius Angelo kwa tuhuma za kupokea rushwa ya zaidi ya shilingi bilioni 1.8 ambazo ni sehemu ya fedha za Escrow.
Watuhumiwa hao wamefikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi kisutu,jijini Dar es Salaam ambapo mara baada ya kusomewa mashitaka yao mahakama imetoa zuio la matumizi ya fedha hizo hadi pale kesi ya msingi itakaposikilizwa na kutolewa hukumu na hilo limekuja baada ya upande wa mashtaka kuiomba mahakama hiyo kutoa zuia hilo.
 
Mtuhumiwa wa kwanza ni Julius Angelo mkurugenzi wa fedha wa benki kuu ya Tanzania BOT ambaye waendesha mashitaka kutoka Takukuru Leornad Swai na Marx Ari wamedai mbele ya hakimu mkazi Devota Kisoka wa mahakama hiyo kuwa Angelo anatuhumiwa kwa shtaka la kupokea rushwa ambapo februari 06 mwaka jana, akiwa jengo la benki ya mkombozi alipokea sh. Milioni 161.7 kupitia akaunti yake.
 
Waendesha mashitaka hao wameieleza mahakama kuwa Angelo alijipatia fedha hizo kutoka kwa James Rugemalira ambaye ni mkurugenzi wa Engineering and Marketing Ltd vip na ambaye pia alikuwa mkurugenzi wa kampuni ya kufua umeme ya Independent Power Tanzania Limited IPTL, kama tuzo ya kusaidia kuidhinisha malipo kutoka kwenye akaunti ya Tegeta Escrow kwenda PAP.
 
Mtuhumiwa huyo amekana shitaka hilo na kutakiwa kuwa na wadhamini wawili watumishi wa serikali watakaosaini bondi ya sh. Milioni 50 kila mmoja na yeye kutakiwa kutoa sh milioni 80 taslim au mali isiyohamishika yenye thamani ya fedha hizo masharti aliyoshindwa kutimiza na kupelekwa rumande hadi januari 27 mwaka huu upande wa mashitaka utakapoanza kutoa maelezo ya awali.
 
Mshitakiwa mwingine ni Stephen Urassa ambaye ni mwanasheria wa shirika la umeme nchini Tanesco ambaye mbele ya hakimu Janeth Karienda waendesha mashitaka hao wa Takukuru wamedai kuwa mtuhumiwa huyo anakabiliwa na kosa la kuomba na kupokea rushwa ya sh milioni 161.7 kwa Rugemalira kama tuzo kwa kuiwakilisha Tanesco na kampuni nyingine zilizokuwa zimeingia mkataba shirika hilo, yuko nje kwa dhamana hadi feb 11 mwaka huu baada ya kutimiza masharti ya dhamana.
 
Mtuhumiwa mwingine ni Kyabukoba Mutabingwa ambaye ni meneja misamaha ya kodi TRA na anatuhumiwa kwa makosa manne ya kupokea rushwa ya zaidi ya sh. Bilioni 1.4 ambapo alikuwa anaiwakilisha tra pamoja na kampuni ya mabibo wine ambapo waendesha mashitaka hao wamedia mbele ya hakimu Janeth kuwa mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo jan 27 mwaka jana ambapo alipokea bilioni 1.6 mwezi huohuo milioni 161.7 na julai 15 alipokea sh milioni 161.7 novemba 14 alipokea sh milioni 161.7.
 
Aidha mtuhumiwa huyo ametakiwa kuwa na wadhamini watatu wanaoaminika ambao kila mmoja atasaini bondi ya shilingi milioni 340 na yeye atoe fedha taslim sh bilioni 1 na ameshindwa kutimiza masharti ya dhamana na kupelekwa rumande hadi jan 29 mwaka huu kesi yake itakapotajwa tena kwa maelezo ya awali.

Share To:
Magpress

MagPress

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

0 comments so far,add yours