Wananchi wa kijiji cha Kisaki tarafa ya Bwakira wilaya ya Morogoro vijijini wamemkataa mwenyekiti wa kijiji hicho Ismail Ng’anja mbele ya kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya na kuzingira ofisi ya kijiji na kutaka kuichoma moto kushinikiza mwenyekiti huyo ajiuzulu kwa madai ya kujihusisha na vitendo vya kupokea pesa za wafugaji wavamizi kwa lengo la kuwapatia maeneo ya kuchungia mifugo.

Wakizungumza kwajazba kwenye mkutano ulioitishwa na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Morogoro kwa lengo la kujadili chanzo cha vurugu zilizosababisha mwenyekiti huyo kupigwa na wananchi wake mnamo Januari 15 mwaka huu wakiwa kwenye mkutano mkuu wa kijiji wananchi hao wamesema hawawezi kuvumilia viongozi wasio waadilifu wanaosababisha migogoro kati ya wakulima na wafugaji na kutaka kamati hiyo iondoke naye vinginevyo wata mshughulikia kwa kumshushia kipigo.

 

Pamoja na katibu tawala wa wilaya ya Morogoro Bwana Alfredi Shayo kujaribu kusuluhisha mgogoro huo kwa kuwashauri wananchi hao kufuata taratibu za kumuondoa mwenyekiti huyo kwa kuitisha mkutano mkuu wa kijiji lakini jitihada hizo zimegonga mwamba jambo ambalo limezua mzozo mkubwa baina ya kamati hiyo na wananchi na mambo yakawa hivi.

 

Baada ya hali ya usalama wa mwenyekiti Ismail kuwa tete huku wananchi wakizingira magari ya kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya mwenyekiti huyo ameamua kujitokeza na kutangaza kijiuzulu wadhifa wake na hapa anasema. 

 

Share To:
Magpress

MagPress

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

0 comments so far,add yours