Serikali mkoani Singida imewaagiza wakurugenzi watendaji wa halmashauri za wilaya pamoja na wakuu wa wilaya wote mkoani Singida, kuhakikisha wanafuatilia miradi inayo anzishwa na iliyo kwisha anza kufanya kazi, ili miradi hiyo iwe endelevu na kuwa saidia wananchi, tofauti na sasa miradi mingi imekuwa haiendelei.
Mkuu wa mkoa wa Singida Dk .Parseko Kone ametoa agizo hilo wakati alipokuwa akiwakabidhi wakuu wa wilaya mashine ishirini nanne  za kufyatulia matofali ( intetlocking blocks ) zilizo tolewa na shirika la nyumba la taifa kwa ajilia ya kusaidia makundi ya vijana kujiajiri.
 
Awali akiongea kwa niaba ya mkurugenzi mkuu wa shirika la nyumba la taifa, meneja wa NHC mkoani Singida Bwana Ladislaus Bamanyisa  amesema shirika la NHC limelenga kupunguza tatizo la makazi hapa nchini ifikapo mwaka elfumbili na kumina tano kwa kujenga nyumba za beinafuu nchi nzima, pia mashine hizo zina lenga kupunguza tatizo la ajira kwa vijana hapa nchini.
 
Akishukuru kwa niaba ya wakuu wa wilaya sita mkoani Singida waliopewa mashine hizo, kiongozi wa wakuu wa wilaya mkoani Singida mwalimu Queen Mlozi ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Singida, amemuhakikishi mkuu wa mkoa mashine hizo pamoja na kuwapatia ajira vijana, zitafanya kazi ya kufyatua matofali bora na kufanikisha kwa kiwango kikubwa opereseni ya ondoa nyumba zilizo ezekwa kwa udongo maarukwa jina tembe
Share To:
Magpress

MagPress

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

0 comments so far,add yours