Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dr. Reginald Mengi amesema iwapo serikali itaandaa mazingira mazuri vijana na Watanzania kwa ujumla wanaweza kujikwamua kiuchumi kwa kutumia akili, juhudi,  na utajiri wa raslimali za taifa.
Mwenyekiti Mtendaji wa IPP DR Reginald Mengi ameyasema hayo jijini Dar es salaam wakati akizindua shindano jipya la kubuni Wazo la Biashara litakaloendeshwa kwa miezi sita mfululizo kuanzia Januari 2015, na kila mwezi mshindi mmoja atajishindia zawadi ya shilingi milioni 10 atakazozitumia kama mtaji wa kutekelezea kwa vitendo wazo lake la biashara.
 
Amesema Shindano hilo linalojulikana kama 3N ikiwa ni kifupisho cha ‘NITABUNI biashara, NITATEKELEZA na NITAFANIKIWA’, litawashirikisha Watanzania pekee na litaendeshwa kwa njia ya mtandao wa kompyuta ambapo mshiriki anatakiwa atatume wazo lake kwa anuani ya twita @regmengi shindano la wazo la biashara.
 
Katika kupata mshindi, jopo maalum la wataalamu watapitia mawazo yatakayowasilishwa na kuteua mawazo 10 bora, na watunzi wa mawazo hayo 10 watafanyiwa usaili kwa njia ya simu ili jopo lijiridhishe kuwa mawazo waliyotoa ni yao binafsi na jinsi walivyojiandaa kuyatekeleza kibiashara. Jopo la wataalamu litamteua mshindi baada ya usaili huo.

Share To:
Magpress

MagPress

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

0 comments so far,add yours