Baadhi ya washiriki wa mkutano huo

..............Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein amesema Zanzibar iko katika juhudi za   kuhakiksiha   inakuwa na madaktari bingwa wa fani mbalimbali wakiwemo wanaohusiana na maradhi  ya mfumo wa utoaji wa haja ndogo  katika kipindi kufupi kijacho.
Dr. Shein ametoa ahadi hiyo wakati akifungua mkutano wa kimataifa wa wataalamu wa maradhi  yanayohusiana na  mfumo wa utoaji  haja ndogo  kutoka Uingereza ambao kwa mwaka huu wameamua kufanya mkutano mkuu hapa zanzibar.
Mkutano huo unaofanyika mkoa wa Kusini Unguja ambapo Dk Shein  amesema serikali yake imepania  na ndio maana imewekeza zaidi katika vyuo vya afya na  kuweka mitaaala maalum katika chuo kikuu cha Zanzibar lengo likiwa ni kupunguza hali ya sasa ambapo daktari mmoja anatibu watu 9700.
Naye Dkt Roger Plail akizungumza kwa niaba ya wataalamu wenzake amesema wataendeleza ushirikaino na madaktari wa  Zanzibar  ambao ndiyo uliowafanya waamue kufanya mkutano  wao Zanzibar.
Katika mkutano huo ambao pia unahudhuriwa na wataalmu wa Zanzibar na Tanzania bara mada mbalimbali ziliweza kujadaliwa na wataaalmu hao..
Mmoja katika magonjwa ambayo  hivi sasa yanaonekana kuzidi kwa kasi hapa nchini ni matattizo ya utoaji wa haja ndogo na kuwepo kwa mkutano huu ni moja ya mikakati ya seriklai  kutafutia dawa  tatizo  hilo.
Share To:
Magpress

MagPress

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

0 comments so far,add yours